Ratiba 16 Bora Ndondo Cup 2025

Ratiba 16 Bora Ndondo Cup 2025

Mashindano ya Ndondo Cup 2025 yamefikia hatua ya 16 Bora, hatua ambayo inatarajiwa kua yenye ushindani mkali na burudani ya aina yake kwa mashabiki wa soka la mitaani. Hii ndiyo hatua inayoleta pamoja vilabu vyenye historia ndefu katika michuano hii na timu changa zenye kiu ya kuandika historia. Ratiba rasmi imetangazwa, ambapo mechi zitaanza 14 Septemba 2025 na kumalizika 19 Septemba 2025.

Kwa mujibu wa Ratiba 16 Bora Ndondo Cup 2025, michezo yote itachezwa katika viwanja viwili maarufu jijini Dar es Salaam ambavyo ni Uwanja wa Kinesi na Uwanja wa Bandari, huku mashabiki wakitarajiwa kujitokeza kwa wingi kushuhudia vipaji vya vijana wakipambana kwa nafasi ya kuingia robo fainali.

Tarehe Timu Zinazokutana Uwanja Saa
14.09.2025 Azimio FC vs Weekend Team Kinesi 10:00 Alasiri
14.09.2025 Mshikamano Talent vs Bahari FC Bandari 10:00 Alasiri
15.09.2025 Buza Mabegani vs Mask FC Bandari 10:00 Alasiri
15.09.2025 Friends Rangers vs Tandika City Kinesi 10:00 Alasiri
18.09.2025 Gomz United vs Haipotei Jogging Bandari 10:00 Alasiri
18.09.2025 Madenge FC vs Keko Furniture Kinesi 10:00 Alasiri
19.09.2025 Mabibo Market vs Kagera Boys Kinesi 10:00 Alasiri
19.09.2025 Soccer City vs Makuburi FC Bandari 10:00 Alasiri

Ratiba 16 Bora Ndondo Cup 2025

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Mashabiki Wa Soka Wakimbizana na Tiketi za Kombe la Dunia 2026
  2. Vituo vya Kununua Tiketi za Siku ya Yanga DAY 2025
  3. Yanga VS Bandari 12/09/2025 Saa Ngapi?
  4. Romain Folz Aitaja Simba Katika Maandalizi ya Mechi ya Yanga na Bandari
  5. Kocha Ken Odhiambo Asema Bandari Imejipanga Kumkabili Bingwa Yanga
  6. Bakari Mwamnyeto Atoa Wito Kwa Mashabiki Kujitokeza Kwa Mkapa
  7. Mbosso Avunja Rekodi za Burudani Simba Day Kwa Performance Bora Zaidi
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo