Ratiba ya Mechi za CRDB Federation Cup Leo 17/02/2026
Michuano ya kombe la shirikisho Tanzania, maarufu kama CRDB Federation Cup (zamani FA Cup), inaendelea kutimua vumbi leo Jumanne, tarehe 17 Februari 2026. Hii ni hatua muhimu ambapo vigogo wa soka nchini na timu zinazochipukia zinachuana vikali kuwania ubingwa na nafasi ya kuiwakilisha nchi kimataifa.
Mechi za Leo: Jumanne, 17 Februari 2026
Leo uwanjani kutakuwa na michezo miwili mikubwa itakayovuta hisia za mashabiki wengi, huku wekundu wa Msimbazi wakishuka dimbani usiku.
KMC FC vs Bandari Tanzania
- Muda: Saa 10:00 Jioni
Simba SC vs Greenland FC
- Muda: Saa 1:00 Usiku
Mechi za Kesho: Jumatano, 18 Februari 2026
Burudani haitaishia leo pekee. Kesho Jumatano, mabingwa watetezi na timu nyingine imara zitakuwa kazini:
JKT Tanzania vs Pan African
- Muda: Saa 10:00 Jioni
Yanga SC vs Cosmopolitan
- Muda: Saa 1:00 Usiku
Mapendekezo ya Mhariri:









Leave a Reply