Kocha wa Simba Steve Barker Atwaa Tuzo ya Kocha Bora Februari 2026
Kocha Mkuu wa Simba Sports Club, Steve Barker, ametwaa tuzo ya Kocha Bora wa mwezi Februari 2026 katika NBC Premier League msimu wa 2025/26, baada ya kuiongoza timu hiyo kupata matokeo mazuri katika michezo ya ligi iliyochezwa ndani ya mwezi huo.
Barker alichaguliwa na Kamati ya Tuzo ya Tanzania Football Federation kufuatia mafanikio ya Simba katika mwezi wa Februari, ambapo timu hiyo ilifanikiwa kushinda michezo miwili na kutoka sare mmoja katika michezo mitatu ya ligi.
Soma Pia
- Yanga Yashindwa Kulenga Lango Dhidi ya Azam FC Licha ya Uwepo wa Depu na Dube
- Bilioni 388.8 Kujenga AFCON City Unguja
- Tanzania Yatoa Zaidi ya Sh80 Bilioni CAF Ili Kuwa Mwenyeji wa AFCON 2027
Matokeo hayo yaliisaidia Simba kupata pointi muhimu zilizoiwezesha kupanda kutoka nafasi ya sita hadi ya tatu katika msimamo wa ligi, hatua iliyochangia kocha huyo kuibuka mshindi wa tuzo hiyo ya kila mwezi.
Katika kinyang’anyiro hicho, Barker aliwashinda makocha wawili waliokuwa wameingia fainali ya tuzo hiyo, ambao ni Pedro Goncalves wa Young Africans Sports Club pamoja na Florent Ibenge wa Azam Football Club.
Uteuzi huo ulifanywa kupitia mchakato wa tathmini ya utendaji wa makocha katika mechi za ligi zilizochezwa ndani ya mwezi wa Februari, ambapo Barker alionekana kuwa na mchango mkubwa katika matokeo chanya ya Simba ndani ya kipindi hicho.
Mapendekezo ya Mhariri:









Leave a Reply