Matokeo ya Darasa la Nne 2024/2025 (NECTA Standard Four Results)
Matokeo ya Darasa la Nne 2024/2025, almaharufu kama NECTA Standard Four Results, ni matokeo ya mtihani wa kitaifa wa wanafunzi wa darasa la nne. Mtihani huu unafanyika kila mwaka katika shule zote ya msingi nchini ili kupima uelewa na maendeleo ya wanafunzi baada ya miaka minne ya elimu ya msingi. Lengo kuu la mtihani huu wa upimaji wa kitaifa ni kutoa tathmini ya kina kuhusu ufahamu wa wanafunzi katika masomo mbalimbali muhimu. Masomo hayo ni pamoja na:
- Lugha ya Kiingereza: Uwezo wa kusoma, kuandika, na kuzungumza Kiingereza.
- Sayansi na Teknolojia: Uelewa wa dhana za kisayansi na uwezo wa kutatua matatizo ya kisayansi na kiteknolojia.
- Maarifa ya Jamii: Ujuzi kuhusu historia, jiografia, na masuala ya kijamii.
- Hisabati: Uwezo wa kutatua matatizo ya hesabu na kutumia dhana za hesabu katika maisha ya kila siku.
- Kiswahili: Uwezo wa kusoma, kuandika, na kuzungumza Kiswahili.
- Uraia na Maadili: Uelewa wa haki na wajibu za uraia pamoja na maadili ya kijamii.
Matokeo haya ni muhimu kwa kutoa mrejesho kwa walimu, wazazi, na serikali kuhusu viwango vya ufanisi wa wanafunzi na kusaidia kuboresha mifumo ya ufundishaji na ujifunzaji.
NECTA Yatangaza Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Nne 2024/2025
Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza rasmi matokeo ya mtihani wa upimaji wa Darasa la Nne leo, Jumamosi Januari 4, 2025. Katika tangazo hilo, NECTA imesema kuwa jumla ya wanafunzi 1,320,227 kati ya wanafunzi 1,530,911 waliofanya mtihani huo wamefaulu, ikiwa ni sawa na asilimia 86.24. Hii ni ongezeko la asilimia 2.9 ikilinganishwa na mwaka uliopita.
Kwa mujibu wa taarifa za NECTA, kati ya wanafunzi waliofaulu, wasichana ni 699,901, sawa na asilimia 53, huku wavulana wakiwa 620,326, sawa na asilimia 47. Hii inaonesha maendeleo katika juhudi za kuinua viwango vya elimu kwa watoto wa kike.
Aidha, NECTA imeripoti kuwa shule 197 kati ya shule 20,036 za msingi zimepata wastani wa Daraja E, ambalo ni daraja la chini zaidi lenye alama kati ya 0 na 60. Hata hivyo, idadi ya shule zilizopata daraja hili imepungua kutoka shule 325 mwaka 2023, jambo linalodhihirisha hatua za kuboresha ubora wa elimu. Wazazi, walimu, na wanafunzi wanashauriwa kupakua matokeo rasmi kupitia tovuti ya NECTA au vituo vyao vya shule ili kupata takwimu sahihi za kina kwa kila mwanafunzi.
Jinsi ya Kuangalia Matokeo ya Darasa la Nne 2024/2025
Baada ya kutangazwa kwa matokeo, wanafunzi, walimu, na wazazi wanaweza kuona matokeo kwa urahisi kwa kutumia njia za kisasa. Matokeo yatapatikana kwenye tovuti rasmi ya NECTA: www.necta.go.tz. Hapa, watumiaji watapata fursa ya kutafuta matokeo kwa mkoa, wilaya, na shule kwa urahisi. Hatua za kuangalia matokeo ni kama ifuatavyo:
- Fungua kivinjari chako na nenda kwenye tovuti rasmi ya NECTA.
- Tembelea sehemu ya “RESULTS” kwenye menyu kuu.
- Chagua “Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa wa Darasa la Nne (SFNA) 2024”.
- Tafuta mkoa wako, kisha chagua wilaya na shule yako ili kuona matokeo.
Umuhimu wa Matokeo ya Darasa la Nne
Matokeo ya Darasa la Nne yana umuhimu mkubwa kwa wanafunzi, wazazi, walimu, na serikali. Baadhi ya umuhimu huu ni pamoja na:
- Kwa Wanafunzi: Matokeo haya yanaweza kuwa kiashiria cha maendeleo ya kitaaluma ya mwanafunzi. Wanafunzi wanaweza kutumia matokeo haya kutambua maeneo ambayo wanahitaji kuboresha na kuweka malengo ya kitaaluma ya baadaye.
- Kwa Wazazi: Matokeo haya yanaweza kusaidia wazazi kuelewa maendeleo ya watoto wao na kuwasaidia katika kufanya maamuzi kuhusu elimu yao ya baadaye.
- Kwa Walimu: Matokeo haya yanaweza kusaidia walimu kutathmini ufanisi wa mbinu zao za kufundisha na kuboresha maeneo ambayo yanaweza kuwa dhaifu.
- Kwa Serikali: Matokeo haya yanaweza kusaidia serikali kutathmini ufanisi wa mfumo wa elimu wa nchi na kuweka mikakati ya kuboresha ubora wa elimu.
Kuelewa Muundo wa Matokeo ya Darasa la Nne 2024 Baada ya kutangazwa
Matokeo haya yanajumuisha vipengele vifuatavyo:
1. Idadi ya Wanafunzi Walioshiriki: Inajumuisha idadi ya wanafunzi waliosajiliwa, waliohudhuria mtihani, na waliokosa.
2. Wastani wa Shule: Kiwango cha ufaulu wa shule nzima kinachotolewa kama daraja (A, B, C, D).
3. Madaraja ya Ufaulu: Wanafunzi hupangiwa madaraja kulingana na alama walizopata:
A: Ufaulu wa hali ya juu.
B: Nzuri sana.
C: Nzuri.
D: Inaridhisha.
Referred: Walioshindwa kufikia kiwango cha ufaulu.
4. Matokeo ya Kila Mwanafunzi: Majina ya mwanafunzi, namba ya mtahiniwa, alama kwa kila somo, na daraja lake vinaoneshwa.
ANGALIA HAPA CHINI MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024
ARUSHA | DAR ES SALAAM | DODOMA |
GEITA | IRINGA | KAGERA |
KATAVI | KIGOMA | KILIMANJARO |
LINDI | MANYARA | MARA |
MBEYA | MOROGORO | MTWARA |
MWANZA | NJOMBE | PWANI |
RUKWA | RUVUMA | SHINYANGA |
SIMIYU | SINGIDA | SONGWE |
TABORA | TANGA |
Mapendekezo ya Mhariri:
- NECTA Matokeo ya Kidato Cha Pili 2024 (Form Two Results)
- Shule Walizopangiwa Darasa la Saba 2025
- Majina ya Wanafunzi na Shule Walizopangiwa Kidato cha Kwanza 2025
- Jinsi ya Kuangalia matokeo ya Darasa la Nne 2024
- Jinsi ya Kuangalia Matokeo ya Kidato Cha Pili 2024
- Matokeo ya Darasa la Nne 2024 Mkoa wa Shinyanga
- Matokeo Ya Darasa La Nne 2024 Kilimanjaro
- Matokeo ya Darasa la Nne 2024 Mkoa wa Tanga
- Matokeo ya Darasa la Nne 2024 Mkoa wa Dodoma
Leave a Reply