Matokeo ya Simba Vs Kagera Sugar Leo 22/06/2025 | Matokeo ya Simba Leo Dhidi ya Kagera Sugar Ligi Kuu
Katika siku ya leo ya Jumapili, jiji la Dar es Salaam linashuhudia hekaheka za kisoka zinazoambatana na matumaini na presha kubwa kutoka kwa mashabiki wa Simba SC. Timu hiyo maarufu ya wekundu wa Msimbazi yenye makao makuu katika viunga vya Kariakoo inatarajiwa kushuka dimbani saa 10:00 jioni (16:00) kuikabili Kagera Sugar, kwenye mchezo wa raundi ya 30 ya Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara msimu wa 2024/2025.
Mechi hii ni ya mwisho kwa Simba kabla ya mtanange wa kukata na shoka dhidi ya watani wao wa jadi, Yanga SC. Ushindi wa leo dhidi ya Kagera Sugar si wa hiari bali ni wa lazima ikiwa Simba inataka kuendeleza matumaini ya kulinyakua taji la ligi kuu msimu huu.
Kwa sasa, Simba SC inashika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kwa alama 75, ikiwa nyuma ya Yanga SC yenye pointi 76. Hii ina maana kuwa matokeo yeyote tofauti na ushindi dhidi ya Kagera Sugar leo yataiweka Simba katika nafasi hatarishi ya kukosa ubingwa hata kabla ya mchezo wa mwisho ambao umekua ukisubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka.
Kocha Fadlu Davids, ambaye ameiongoza Simba kwa mafanikio tangu atue kutoka Raja Casablanca, amesema kuwa wachezaji wake wako tayari kwa mapambano. Amesisitiza umuhimu wa kutumia nafasi vizuri, akiwataka washambuliaji wake akina Jean Charles Ahoua, Ellie Mpanzu na Steven Mukwala kuonyesha ubora wao.
Ingawa Kagera Sugar tayari imeshuka daraja msimu huu, kocha wa Simba amekataa kubeza wapinzani wake. “Timu ambazo zimeshuka daraja hucheza kwa uhuru zaidi—hazina presha ya alama. Hivyo ni hatari zaidi,” alisema Fadlu.
Katika mechi zake za karibuni, Kagera imeonyesha mapungufu makubwa—ikitoka sare dhidi ya Namungo FC na kupoteza michezo mingine mitatu. Hii inatoa picha ya timu iliyo dhaifu kwa upande wa matokeo, lakini ambayo inaweza kuleta mshangao iwapo itapewa nafasi.
Matokeo ya Simba Vs Kagera Sugar Leo 22/06/2025
Simba SC | vs | Kagera Sugar |
Rekodi za Hivi Karibuni: Simba SC na Kagera Sugar
Matokeo ya karibuni ya Simba SC:
- 18 Juni: KenGold 0-5 Simba SC
- 28 Mei: Simba SC 1-0 Singida Black Stars
- 11 Mei: KMC 1-2 Simba SC
- 2 Mei: Simba SC 2-1 Mashujaa
Matokeo ya karibuni ya Kagera Sugar:
- 18 Juni: Namungo FC 0-0 Kagera Sugar
- 12 Mei: Kagera Sugar 0-1 Mashujaa
- 9 Aprili: Dodoma Jiji FC 2-0 Kagera Sugar
Takwimu hizi zinaonyesha Simba SC iko katika kiwango bora zaidi kwa sasa, ikiwa imeshinda michezo yake yote mitatu ya mwisho kwa tofauti kubwa ya mabao.
Mchezo wa Simba Vs Kagera Sugar Leo 22/06/2025 una uzito mkubwa kwa Simba SC, ambayo inalenga kutunza matumaini ya ubingwa hadi dakika ya mwisho ya msimu. Kwa Kagera Sugar, huu ni mchezo wa heshima na nafasi ya kuwa kikwazo kwa timu kubwa.
Endelea kufuatilia ukurasa huu kwa sasisho la moja kwa moja kuhusu kikosi rasmi na hatimaye Matokeo ya Simba Vs Kagera Sugar Leo 22/06/2025 mara baada ya kipenga cha mwisho.
Mapendekezo ya Mhariri:
- Kikosi cha Simba Vs Kagera Sugar Leo 22/06/2025
- Simba Vs Kagera Sugar Leo 22/06/2025 Saa Ngapi?
- Yanga vs Dodoma Jiji Leo 22/06/2025 Saa Ngapi?
- TFF Yafunga Rasmi Zoezi la Uchukuaji wa Fomu za Uongozi – Wagombea 25 Wajitokeza
- Tanzania Yashinda Ubingwa wa CECAFA Wanawake 2025 Kupitia Twiga Stars
- KMKM Mabingwa wa FA Cup Zanzibar 2025 Baada ya Ushindi wa 4-2 Dhidi ya Chipukizi
- Timu Zilizofuzu Hatua ya 16 Bora Kombe la Dunia la Vilabu 2025
- Klabu ya Liverpool Yamwaga Mamilioni Kumnasa Florian Wirtz
- Viingilio Simba SC vs Kagera Sugar 22/06/2025
Leave a Reply