Matokeo ya Darasa La Nne 2025 Mkoa wa Geita

Matokeo ya Darasa La Nne 2025 Mkoa wa Geita

Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) leo Jumamosi tarehe 10 Januari 2026 limetangaza rasmi Matokeo ya Darasa la Nne 2025, matokeo ya mtihani wa kitaifa ulihusisha wanafunzi wa shule za msingi kutoka mikoa yote nchini, wakiwemo wanafunzi wa Mkoa wa Geita.

Mtihani huu wa Darasa la Nne ulifanyika kuanzia tarehe 10 Novemba 2025 hadi 20 Novemba 2025 kama sehemu ya Upimaji wa Kitaifa unaolenga kutathmini kiwango cha ufahamu na maendeleo ya wanafunzi baada ya miaka minne ya elimu ya msingi.

Matokeo ya Darasa La Nne 2025 Mkoa wa Geita

Matokeo ya Darasa la Nne 2025/2026 ni Nini?

Matokeo ya Darasa la Nne 2025/2026, yanayojulikana pia kama NECTA Standard Four Results, ni matokeo ya mtihani wa kitaifa unaofanywa kila mwaka kwa wanafunzi wa darasa la nne katika shule zote za msingi nchini. Mtihani huu hulenga kupima kiwango cha uelewa wa wanafunzi katika masomo muhimu yanayounda msingi wa elimu ya awali.

Masomo yaliyopimwa ni pamoja na:

  1. Lugha ya Kiingereza – Uwezo wa kusoma, kuandika na kuzungumza
  2. Sayansi na Teknolojia – Uelewa wa dhana za kisayansi na kiteknolojia
  3. Maarifa ya Jamii – Historia, jiografia na masuala ya kijamii
  4. Hisabati – Utatuzi wa matatizo ya kihesabu na matumizi ya hesabu katika maisha ya kila siku
  5. Kiswahili – Kusoma, kuandika na kuzungumza
  6. Uraia na Maadili – Haki, wajibu na maadili ya kijamii

Matokeo haya hutoa mrejesho muhimu kwa walimu, wazazi na serikali kuhusu ufanisi wa mfumo wa ufundishaji na ujifunzaji.

Jinsi ya Kuangalia Matokeo ya Darasa la Nne 2025 Mkoa wa Geita

Baada ya Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) kutangaza rasmi Matokeo ya Darasa la Nne 2025, wanafunzi, wazazi na walimu wa Mkoa wa Geita sasa wanaweza kuyatazama matokeo hayo moja kwa moja kupitia tovuti rasmi ya NECTA.

Mfumo huu wa upatikanaji wa matokeo umewekwa ili kuhakikisha taarifa sahihi na zilizothibitishwa zinawafikia wahusika wote kwa urahisi, kulingana na shule na vituo vya mitihani vilivyoshiriki mtihani huo.

Hatua za Kuangalia Matokeo ya Darasa la Nne 2025 Kupitia Tovuti Rasmi ya NECTA

NECTA huchapisha matokeo ya mtihani wa Darasa la Nne kwa mikoa yote kwenye tovuti yake rasmi mara tu baada ya kuyathibitisha.

Fuata hatua zifuatazo uweze kutazama matokeo yako:

  1. Fungua kivinjari cha mtandao kwenye simu au kompyuta
  2. Tembelea tovuti rasmi ya NECTA: www.necta.go.tz
  3. Bonyeza sehemu ya “RESULTS” kwenye menyu kuu
  4. Chagua Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa wa Darasa la Nne (SFNA) 2025
  5. Chagua Mkoa wa Geita
  6. Bonyeza jina la wilaya husika
  7. Tafuta shule au namba ya kituo ili kuona matokeo

Ili kukurahisishia zoezi zima la kuangalia Matokeo ya Darasa la Nne 2025 Mkoa wa Geita, hapa chini tumekuandalia jedwali lenye viungo vya moja kwa moja vitakavyokuwezesha kufikia matokeo ya Darasa la Nne kwa haraka kupitia tovuti rasmi ya Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA). Kupitia viungo hivi, utapelekwa moja kwa moja kwenye ukurasa wa matokeo kulingana na wilaya husika.

Ili kutazama matokeo, bofya jina la wilaya ambayo shule uliyofanyia mtihani ipo.

BUKOMBE

CHATO

GEITA

GEITA TC

MBOGWE

NYANG’HWALE

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Matokeo ya Darasa la Nne 2025 (NECTA Standard Four Results)
  2. NECTA Matokeo ya Kidato Cha Pili 2025 (Form Two Results)
  3. NECTA Yatangaza Usajili wa Watahiniwa wa Kujitegemea CSEE na FTNA 2026
  4. Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2025/2026 NECTA
  5. Fomu za Kujiunga Vyuo Vya VETA 2026
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo