Nafasi Mpya za Kazi MDAs & LGAs Juni 2025 – Tangazo la Ajira Serikalini Nafasi 6,732

Nafasi Mpya za Kazi MDAs & LGAs Juni 2025 | Ajira MDAs & LGAs 2025

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, kwa niaba ya Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGAs) na Taasisi za Serikali (MDAs), anakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza jumla ya nafasi 6,732 kama ilivyoainishwa katika tangazo hili la ajira la Juni 2025. Hii ni fursa adhimu kwa Watanzania wanaotafuta ajira katika sekta ya umma, hasa katika nyanja za afya, elimu, na utawala. Sekretarieti ya Ajira imebainisha nafasi mbalimbali zinazopatikana kwenye mamlaka tofauti nchini – ikilenga kukuza utoaji wa huduma bora kwa wananchi kupitia kuongeza watumishi wenye sifa na weledi.

Nafasi Mpya za Kazi MDAs & LGAs Juni 2025 – Tangazo la Ajira Serikalini Nafasi 6,732
Nafasi Mpya za Kazi MDAs & LGAs Juni 2025 – Tangazo la Ajira Serikalini Nafasi 6,732

Orodha Kamili ya Nafasi za Kazi Zilizotangazwa MDAs & LGAs Juni 2025

Nafasi Za Kazi MDAs & LGAs Juni 2025 Kada ya Afya

  1. Daktari Bingwa wa Watoto Daraja la II (Medical Specialist – Pediatrician II) – Nafasi 3
  2. Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani Daraja la II (Medical Specialist – Internal Medicine II) – Nafasi 2
  3. Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wakina Mama (Medical Specialist – Gynaecologist) – Nafasi 17
  4. Daktari Bingwa wa Upasuaji Daraja la II (Medical Specialist – General Surgeon II) – Nafasi 10
  5. Daktari Bingwa wa Masikio, Pua na Koo Daraja la II (Medical Specialist – Ear, Nose and Throat II) – Nafasi 2
  6. Daktari Bingwa wa Usingizi Daraja la II (Anesthesia II) – Nafasi 1
  7. Daktari Daraja la II (Medical Officer II) – Nafasi 383
  8. Mfamasia Daraja la II (Pharmacist II) – Nafasi 124
  9. Mhandisi Vifaa Tiba Daraja la II (Biomedical Engineer II) – Nafasi 40
  10. Daktari Bingwa wa Meno Daraja II (Dental Specialist) – Nafasi 4
  11. Daktari wa Upasuaji wa Kinywa na Meno Daraja la II (Dental Surgeon II) – Nafasi 186
  12. Afisa Muuguzi Daraja la II (Nursing Officer II) – Nafasi 250
  13. Afisa Muuguzi Msaidizi Daraja la II (Assistant Nursing Officer II) – Nafasi 4,015
  14. Fiziotherapia Daraja la II (Physiotherapist II) – Nafasi 67
  15. Mteknolojia Msaidizi (Dawa) – Nafasi 30
  16. Msaidizi Lishe (Nutrition Assistant) – Nafasi 10
  17. Tabibu Msaidizi Daraja la II (Clinical Assistant II) – Nafasi 582
  18. Tabibu wa Kinywa na Meno Daraja la II (Dental Therapist II) – Nafasi 193
  19. Afisa Afya Mazingira Daraja la II (Environmental Health Officer II) – Nafasi 147
  20. Afisa Afya Mazingira Msaidizi Daraja la II (Assistant Environmental Health Officer II) – Nafasi 396
  21. Afisa Fiziotherapia Daraja la II (Physiotherapy Officer II) – Nafasi 12
  22. Mteknolojia wa Radiografia Daraja II – Radiolojia (Radiography Technologist II – Radiology) – Nafasi 13
  23. Dobi (Launderer) – Nafasi 56
  24. Mpishi (Cook) – Nafasi 14

Nafasi Za Kazi MDAs & LGAs Juni 2025 Kada ya Elimu

  1. Mwalimu Daraja la III B – Hisabati (Mathematics) – Nafasi 150

Nafasi Za Kazi MDAs & LGAs Juni 2025 Kada ya Uchumi na Mipango

  1. Mchumi Daraja la II (Economist II) – Nafasi 30

Sifa na Masharti Muhimu Kwa Waombaji Wa Nafasi Mpya za Kazi MDAs & LGAs Juni 2025

Kabla ya kutuma maombi, waombaji wanapaswa kuzingatia masharti yafuatayo:

  • Uraia na Umri: Mwombaji lazima awe Mtanzania mwenye umri usiozidi miaka 45.
  • Watu wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na kutaja aina ya ulemavu kwenye mfumo wa maombi.
  • Vyeti vya Kuzaliwa: Cheti cha kuzaliwa lazima kiwe kimehakikiwa na Mwanasheria/Wakili.
  • Wasifu wa Maisha (CV): Waombaji waambatishe CV iliyoandikwa kwa ufasaha ikionyesha anwani, namba ya simu, na majina ya wadhamini watatu.
  • Vyeti vya Elimu: Ni lazima kuambatisha nakala zilizothibitishwa za vyeti vya taaluma, kuanzia kidato cha nne hadi taaluma husika (Stashahada, Shahada n.k).
  • Vyeti Vinavyokubalika: Hakutakubaliwa result slip, provisional results, au testimonials.
  • Vyeti vya Nje ya Nchi: Wahitimu wa masomo ya nje ya Tanzania wanapaswa kuhakikisha vyeti vimehakikiwa na TCU, NACTE au NECTA.
  • Wastaafu na Watumishi wa Serikali: Wastaafu hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kwa kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi. Aidha, watumishi walioko katika nafasi za kuingilia hawapaswi kuomba.
  • Maombi ya Kughushi: Taarifa au sifa za kughushi zitachukuliwa hatua kali za kisheria.
  • Mwisho wa Maombi: Tuma maombi yako kabla au ifikapo tarehe 26 Juni, 2025.

Namna ya Kutuma Maombi

Waombaji wote wanatakiwa kutuma maombi kupitia mfumo wa kielektroniki wa Ajira (Recruitment Portal) kwa kutumia anuani:

🔗 http://portal.ajira.go.tz/

➡ Maombi yote yatakayowasilishwa nje ya mfumo huu hayatafanyiwa kazi.

MUHIMU: Maombi yote ya Nafasi Mpya za Kazi MDAs & LGAs Juni 2025 lazima yaambatane na barua ya maombi iliyosainiwa, vyeti vya elimu vilivyohakikiwa, na iwe imetumwa kwa anuani ifuatayo:

  • KATIBU,
  • OFISI YA RAIS,
  • SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA,
  • S. L. P. 2320,
  • DODOMA.

Kwa jumla, tangazo hili la ajira linatoa nafasi kwa maelfu ya Watanzania kujipatia ajira serikalini katika kada muhimu zinazogusa maisha ya wananchi moja kwa moja. Kama una sifa stahiki, usikose kutuma maombi yako mapema kabla ya tarehe ya mwisho – 26 Juni 2025.

Kwa taarifa zaidi, Pakua na Soma Tangazo Rasmi la Ajira Hizi Hapa Chini

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Mfano wa Barua ya Maombi ya Kazi Jeshi la JWTZ
  2. Mfano wa Barua ya Maombi ya Kazi Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ)
  3. Rais Samia Atangaza Ongezeko Kubwa la Mishahara kwa Watumishi wa Umma
  4. Kiwango Cha Chini Cha Mshahara Kwa Watumishi wa Umma Chapanda Hadi 500,000
  5. Ratiba ya Usaili Wa Mahojiano TRA 2025
  6. Majina ya Walioitwa Kwenye Usaili Jeshi la Polisi Tanzania April 2025
  7. Matokeo ya Usaili TRA April 2025, Majina ya Waliofaulu Usaili TRA 2025
  8. Majina Ya WALIOITWA Kwenye Usaili Jeshi La Zimamoto Na Uokoaji 2025
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo