Yanga Kususia Fainali CRDB FA Cup Kisa Madeni ya Msimu Uliopita
Afisa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Yanga, Ally Kamwe, ametangaza kwa msisitizo kuwa mabingwa hao wa kihistoria wa Tanzania hawatashiriki katika mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB (CRDB FA Cup) unaotarajiwa kuchezwa Juni 28, 2025, endapo hawatalipwa fedha zao za ushindi wa msimu uliopita.
Katika taarifa kali iliyotolewa na Kamwe kutoka makao makuu ya klabu hiyo, alieleza kuwa Yanga imevumilia kwa muda mrefu dharau na kutokujali kutoka kwa mamlaka husika, lakini sasa imefika mwisho.
“Taarifa hii iwafikie Ofisi ya Katibu Mkuu wa TFF na Wadhamini wa mashindano ya Kombe la Shirikisho la CRDB, kuwa hatutacheza mchezo wa Fainali wa CRDB siku ya tarehe 28, mpaka tutakapolipwa hela yetu ya ubingwa kwa msimu uliopita,” alisema Kamwe kwa ukali.
Sakata la Madeni Linaloikabili TFF
Kamwe aliibua tuhuma mpya zinazohusiana na fedha ambazo klabu ya Yanga inadai baada ya kutwaa ubingwa wa Kombe la FA msimu uliopita, walipoiangusha Azam FC kwa changamoto ya mikwaju ya penalti katika Uwanja wa New Amaan, Zanzibar. Hadi sasa, Yanga haijapata malipo yake licha ya kushinda taji hilo kihalali.
Kamwe alifafanua kuwa licha ya juhudi za klabu hiyo kuwasiliana na mamlaka husika kupitia barua mbalimbali, hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa na TFF wala waandaaji wa mashindano.
“Tumevumilia vya kutosha, tumechoka kuandika barua kila wakati tukikumbusha kuhusu fedha hizi, sasa tumeona tutoke hadharani tuyaweke wazi ili watu wajue,” alisema kwa uchungu.
Yanga Yasimama Kidete: Msimamo wa Kutocheza
Sio tu kuhusu mchezo wa fainali ya FA, bali Kamwe alithibitisha kuwa klabu hiyo imefikia hatua ya kuchukua msimamo mkali zaidi, ikiwa ni pamoja na kutoshiriki hata mchezo wa watani wa jadi, yaani Kariakoo Dabi dhidi ya Simba SC. Hili linakuja baada ya kile kinachodaiwa kuwa ni kupuuzwa kwa matakwa halali ya klabu hiyo.
Matakwa hayo manne yaliyoainishwa na Kamwe ni pamoja na:
- Kuvunjwa kwa Kamati ya Usimamizi ya Ligi – Yanga inadai kamati hiyo imeshindwa kusimamia ligi kwa weledi msimu wa 2024/2025.
- Kujiuzulu kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Almas Kasongo – Klabu inamtuhumu kwa kupotosha kuhusu kuahirishwa kwa mechi yao dhidi ya Simba.
- Kujiuzulu kwa Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidao – Kutokana na lawama nyingi dhidi ya waamuzi, ambao licha ya makosa, wameendelea kupewa mechi kubwa.
- Kuundwa kwa Bodi Huru ya Kusimamia Ligi – Hili ni takwa la muda mrefu ambalo Yanga inasema linaweza kuamua kama wataendelea kushiriki ligi ijayo au la.
Mapendekezo ya Mhariri:
- Matokeo Afrika Kusini vs Taifa Stars Leo 06/06/2025
- Afrika Kusini vs Taifa Stars Leo 06/06/2025 Saa Ngapi?
- Herry Sasii Afungiwa Soka Miezi 6 Kisa Mechi ya Simba na Singida
- Seif Karihe Acharazwa Faini na Kufungiwa Michezo Mitatu kwa Kurusha Chupa
- Ronaldo Aipeleka Ureno Fainali UEFA Nations League 2024/2025
Leave a Reply