Matokeo ya Yanga vs Wiliete SC Leo 27/09/2025
Safari ya kusaka tiketi ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika CAF inaendelea kwa kishindo. Wikiendi hii macho ya mashabiki wa soka Tanzania yameelekezwa jijini Dar es Salaam, ambapo Young Africans SC (Yanga) watashuka dimbani kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa kuwakabili Wiliete SC ya Angola katika mchezo wa marudiano.
Mabao matatu waliyoibuka nayo ugenini wiki iliyopita yamewapa nafasi kubwa ya kufuzu hatua inayofuata, lakini mchezo wa leo, Jumamosi 27 Septemba 2025, utakuwa kipimo cha kuthibitisha ubora wao mbele ya mashabiki wao wa nyumbani.
Mashabiki wa Yanga Sc wanatarajia kuona timu yao ikikamilisha kazi iliyoanzishwa Benguela. Kocha Romain Folz ameweka wazi kuwa kikosi chake hakitategemea matokeo ya awali pekee, bali kitaingia na lengo la kushinda tena nyumbani.
Kwa upande mwingine, Wiliete SC chini ya kocha Bruno Ferry wamesema hawatakuja “kupaki basi.” Badala yake, watajaribu kushambulia mwanzo hadi mwisho ili kupata mabao ya mapema yanayoweza kubadili matokeo ya jumla.
Matokeo ya Yanga vs Wiliete SC Leo 27/09/2025
Yanga Sc | 2-0 | Wiliete SC |
Taarifa Kuhusu Mechi
🏆 #CAFCL
🆚 Wiliete SC
🗓️ 27 Sept 2025
🏟️ Benjamin Mkapa
⏱️ Saa 11:00 Jioni
Umuhimu wa Mechi ya Leo
Mshindi wa jumla kati ya Yanga vs Wiliete SC ataendelea kwenye raundi inayofuata kuwania tiketi ya hatua ya makundi. Huko atakutana na mshindi kati ya Elgeco Plus ya Madagascar na Silver Striker ya Malawi.
Kwa Yanga, hii ni nafasi muhimu ya kuendeleza safari yao kwenye michuano mikubwa barani Afrika, kuongeza heshima ya klabu na kuonyesha ubora wa soka la Tanzania.
Form ya Yanga Kabla ya Mchezo
Kabla ya marudiano ya leo, Yanga imecheza michezo mitatu ya mashindano msimu huu na haijaruhusu bao lolote:
- Ushindi 1-0 dhidi ya Simba SC (Ngao ya Jamii).
- Ushindi 3-0 dhidi ya Wiliete SC (mchezo wa kwanza).
- Ushindi 3-0 dhidi ya Pamba Jiji (Ligi Kuu NBC).
Hali hii inawapa mashabiki matumaini kwamba kikosi kipo imara kutafuta ushindi mwingine nyumbani.
Mapendekezo ya Mhariri:
- Yanga vs Wiliete SC Leo 27/09/2025 Saa Ngapi?
- Kikosi cha Yanga vs Wiliete SC Leo 27/09/2025
- KMKM Yatinga Raundi ya Pili ya CAF Baada ya Kuichapa AS Port ya Djibouti
- Viingilio Mechi ya Yanga vs Wiliete SC 27/09/2025
- Sergio Busquets Atangaza Kustaafu Soka Mwishoni Mwa Msimu Huu
- Kocha Folz Aahidi Ushindi Mkubwa Mechi ya Marudiano Dhidi ya Wiliete
- Yanga SC Yazindua Jezi Mpya Ili Kulinda Mapato Dhidi ya Jezi Feki
- Msimamo wa Ligi kuu NBC Tanzania 2025/2026
- Wafungaji Bora Ligi Kuu ya NBC Tanzania 2025/2026
Leave a Reply