Timu Zilizofuzu 16 Bora Kombe la Shirikisho la CRDB Federation Cup 2024/2025
Michuano ya Kombe la Shirikisho la CRDB Bank Federation Cup 2024/2025, maarufu kama Kombe la FA Tanzania, inaendelea kushika kasi huku hatua ya 16 bora ikikaribia. Timu zimekuwa zikishindana vikali kuhakikisha zinapata nafasi ya kusonga mbele, na tayari baadhi yao zimejihakikishia tiketi ya hatua inayofuata baada ya kuonyesha uhodari wao katika raundi ya nne ya mashindano haya.
Timu Zilizofuzu Hatua ya 16 Bora CRDB Federation Cup 2024/2025
Mashindano ya CRDB Bank Federation Cup yanaendelea kwa ushindani mkubwa, huku timu 16 zikifanikiwa kufuzu hatua ya 16 bora baada ya kushinda michezo yao. Timu zilizofuzu ni kama ifuatavyo:
- Tabora United
- Kagera Sugar
- Mashujaa FC
- Pamba Jiji FC
- Stand United
- Giraffe FC
- Yanga SC
- Simba SC
- Big Man
- Songea United
- Singida Black Stars
- Mbeya City
- Mtibwa Sugar
- KMC FC
- JKT Tanzania
- Mbeya Kwanza
Muhtasari wa Mechi za Raundi ya Nne (02/03/2025)
Katika michezo iliyochezwa Machi 2, 2025, timu mbalimbali zilionyesha uwezo wao, huku baadhi zikifuzu kwa mikwaju ya penalti baada ya sare katika muda wa kawaida wa mchezo. Hapa ni matokeo ya mechi hizo:
- Cosmopolitan FC 0-2 KMC FC (KMC Complex, DSM)
- Tanzania Prisons 1-1 BigMan FC (BigMan FC ilishinda kwa penalti 3-2) (Mabatini, Pwani)
- Singida BS 4-0 Leo Tena FC (CCM Liti, Singida)
- Azam FC 1-1 Mbeya City (Mbeya City ilishinda kwa penalti 4-2) (Azam Complex, DSM)
Mapendekezo ya Mhariri:
- Ratiba ya Kombe la Shirikisho la CRDB Federation Cup Leo 03/03/2025
- Ratiba ya Mechi za Simba Machi 2025
- Mbeya City Yaing’oa Azam CRDB Bank Federation Cup kwa Mikwaju ya Penati
- Simba Yaivuruga Rekodi ya Mwambusi Arusha
- Amrouche Atangazwa Kocha Mpya wa Timu ya Taifa ya Rwanda
- Baraka Majogoro Karibu Kujiunga na Orlando Pirates
- Hat Trick Dhidi ya Coastal Yampa Mukwala Mzuka Kuelekea Dabi ya Kariakoo
Leave a Reply