Aina ya Vifurushi Vya Bima ya Afya NHIF kwa Mtu Binafsi; Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) unatoa vifurushi mbalimbali vya bima ya afya kwa mtu binafsi, ambavyo vinalenga kutoa uhakika wa matibabu kwa kila mwanachama. Vifurushi hivi vimeundwa kwa namna ambayo vinaweza kukidhi mahitaji ya kiafya ya watu wa kada tofauti, huku vikitoa viwango tofauti vya huduma kulingana na gharama ya kifurushi husika. Vifurushi hivi ni pamoja na Najali Afya, Wekeza Afya, na Timiza Afya.
Aina ya Vifurushi Vya Bima ya Afya NHIF kwa Mtu Binafsi
Serengeti Afya
Kifurushi hiki kinatoa wigo mpana wa huduma za matibabu, ikiwemo:
- Huduma za madaktari wa kawaida, bingwa, na bingwa bobezi.
- Vipimo vya kina kama CT-Scan, MRI, Ultra Sound, na X-ray.
- Matibabu ya magonjwa sugu kama kisukari, shinikizo la damu, na magonjwa ya moyo.
- Huduma za uzazi, upasuaji mkubwa na mdogo, pamoja na matibabu ya saratani (dawa na mionzi tiba).
- Huduma za meno, utengamao, na vifaa tiba pandikizi.
Ngorongoro Afya
Hiki ni kifurushi kinacholenga huduma za msingi na baadhi ya huduma za kibingwa, ikiwemo:
- Huduma za madaktari wa kawaida na bingwa.
- Vipimo vya maabara, CT-Scan, na Ultra Sound.
- Matibabu ya magonjwa sugu na baadhi ya magonjwa ya saratani.
- Huduma za uzazi na baadhi ya upasuaji mdogo.
Viwango vya Michango kwa Wanachama wa Bimba ya Afya ta NHIF
Kiwango cha mchango kinategemea ukubwa wa familia na kifurushi kinachochaguliwa. Kwa mfano:
- Serengeti Afya: Kuanzia TZS 660,000 kwa mtu mmoja mwenye umri wa miaka 18-35.
- Ngorongoro Afya: Kuanzia TZS 240,000 kwa mtu mmoja mwenye umri wa miaka 0-17.
Jinsi ya Kujisajili na Vifurushi Vya Bima ya Afya NHIF 2024
- Mwanachama anatakiwa kujaza fomu ya kujiunga ambayo inapatikana katika ofisi za Mfuko nchi nzima au kupitia tovuti ya Mfuko www.nhif.or.tz
- Mwanachama anatakiwa kuwa na namba ya kitambulisho cha Taifa
- Mwanachama atapaswa kuwa na picha moja ya rangi ya ukubwa wa passport size.
- Mwanachama anayemwandikisha mwenza atahitajika kuambatanisha picha moja ya mwenza ya rangi, nakala ya cheti cha ndoa pamoja na namba ya kitambulisho cha Taifa.
- Mwanachama anayemwandikisha mtoto kama mtegemezi atahitajika kuambatanisha picha ya mtoto na nakala ya cheti cha kuzaliwa cha mtoto. Tangazo la kuzaliwa linaweza kuwasilishwa kama mbadala wa cheti cha kuzaliwa endapo mtoto ana umri wa chini ya miezi 6.
- Mwanachama atapewa namba ya malipo (control number) ambayo ataitumia kufanya malipo kupitia benki au mitandao ya simu.
- Mwanachama atafanya malipo yote kwa mkupuo au kwa awamu kupitia utaratibu maalum wa benki.
- Mwanachama atapatiwa kitambulisho cha matibabu na kuanza kupata huduma zilizoainishwa katika kifurushi alichokichagua kwa kuzingatia vigezo na masharti yaliyowekwa.
- Mwanachama anaweza kujisajili kupitia mtandao, ili kujisajili tembelea tovuti ya Mfuko www.nhif.or.tz ukiwa na namba ya kitambulisho cha Taifa ili kukamilisha usajili wako.
Mapendekezo ya mhariri:
Leave a Reply