Ratiba ya Nusu Fainali Kombe la Muungano 2026

Ratiba ya Nusu Fainali Kombe la Muungano 2026

Michuano ya robo fainali ya Kombe la Muungano 2026 imefikia tamati rasmi kufuatia kukamilika kwa mechi zote zilizokuwa zikiamua hatma ya timu kuelekea hatua inayofuata. Mchezo wa mwisho ulihusisha Simba SC dhidi ya Mafunzo FC, ambapo matokeo yake yamekamilisha orodha ya timu nne bora zilizofuzu. Sasa macho ya wadau wa soka yanaelekezwa kwenye hatua ya nusu fainali, inayotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na ubora wa vikosi vilivyofanikiwa kusonga mbele.

Hatua hii imezikutanisha baadhi ya timu zenye historia na ushindani mkubwa, hali inayoongeza hamasa kuelekea mechi zijazo za kuwania tiketi ya fainali.

Ratiba ya Nusu Fainalu Kombe la Muungano 2026

Timu Zilizofuzu Nusu Fainali Muungano Cup 2026

Baada ya michezo ya robo fainali, timu nne zimefanikiwa kusonga mbele na kuthibitisha ubabe wao ndani ya dimba la New Amaan Complex, Zanzibar:

  • Simba SC – ilitinga nusu fainali kwa ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Mafunzo FC
  • Mlandege FC – iliiondoa Singida Black Stars kwa ushindi wa mabao 2-1
  • Yanga SC – ilionesha ubora mkubwa kwa ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Muembe Makumbi City
  • Azam FC – iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya KVZ, mabao yote yakifungwa na Jean Ngita

Matokeo haya yameweka msingi wa mechi kali katika hatua inayofuata, huku kila timu ikiwa na lengo la kufika fainali.

Ratiba ya Nusu Fainali Kombe la Muungano 2026

Ratiba rasmi ya mechi za nusu fainali imepangwa kama ifuatavyo:

Aprili 25, 2026 – Saa 2:15 Usiku

  • Azam FC vs Yanga SC

Aprili 26, 2026 – Saa 2:15 Usiku

  • Mlandege FC vs Simba SC

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Ratiba ya Kombe la Muungano Leo 23/04/2026
  2. Timu Zilizofuzu Nusu Fainali Kombe la Muungano 2026
  3. Vilabu Bora Afrika 2026/2027 (CAF Club Ranking)
  4. CAF Rankings 2026: Simba Yaporomoka, Yanga Yaendelea Kung’ara Afrika
  5. Mshindi wa Kombe la Muungano Kubeba Kitita Cha Sh150 Milioni
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo